Tuesday, February 12, 2013

Kamati kuu ya CCM yatajwa

Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi katika kikao chake cha siku mbili Februari 10 na 11, 2013 kilichofanyika mjini Dodoma, pamoja na mambo mengine kimeridhia uteuzi na kufanya uchaguzi wa Wajumbe 14 wa Kamati Kuu yake. 

Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imeridhia uteuzi wa Dokta Salim Ahmed Salim kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu kupitia nafasi 10 za uteuzi wa Mwenyekiti wa CCM. 

Wajumbe 14 waliochaguliwa kuwa wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ni:-

Wajumbe wa Kamati Kuu - Bara 
1. Ndugu Pindi Chana 
2. Ndugu Adam Kimbisa 
3. Ndugu William Lukuvi 
4. Dokta Emmanuel Nchimbi 
5. Ndugu Jerry Slaa 
6. Profesa Anna Tibaijuka
7. Ndugu Stephen Wassira 

Wajumbe wa Kamati Kuu - Zanzibar 
1. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha
 2. Ndugu Hussein Mwinyi 
3. Pofesa Makame Mbarawa Mnyaa 
4. Dokta Salim Ahmed Salim 
5. Ndugu Maua Daftari. 
6. Ndugu Samia Suluhu Hassan 
7. Ndugu Hadija H. Aboud 

 Imetolewa na:- Nape Moses Nnauye, 
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA ITIKADI NA UENEZI 

12/02/2013

No comments: